Kumbe kuna Marais wanaoomba kupunguziwa muda wa kukaa madarakani..!
Tuliona machafuko ya Burkina Faso ambayo yalitokana na ishu ya aliyekuwa Rais wa nchi hiyo, Blaise Compaoré
 kutaka kulishawishi Bunge ili limuongezee muda wa kukaa madarakani, iko
 ishu ya Congo DRC pia kwa sasa ambapo hali si shwari kutokana na 
machafuko ambayo yalianza baada ya Serikali ya nchi hiyo kutaka kufanya 
sensa ya watu na kusogeza mbele muda wa kufanya Uchaguzi Mkuu.
Stori 
za viongozi wa Afrika kujiongezea muda wa kukaa madarakani ni kawaida 
kusikika, lakini kusikia kwambe eti Rais wa nchi anaomba kupunguziwa 
muda wa kukaa madarakani hii imekaa tofauti mtu wangu!
Rais wa Senegal, Macky Sall amependekeza
 ipigwe kura ya maoni ambayo itafanya kuwe na mabadiliko ya Katiba 
ambayo yatafanya muda wake wa kukaa madarakani upungue kutoka miaka saba
 kwa muhula mmoja wa uongozi mpaka miaka mitano.
Rais 
huyo amesema alichaguliwa kwa miaka saba lakini mwakani mwezi Mei 
anapendekeza kufanyika kwa kura ya maamuzi ili kupunguza kwa muda wake 
na kupisha wengine waendelee na nafasi hiyo.
Kama hili likitimia Rais Sall atakuwa
 ametimiza moja ya ahadi aliyoahidi wakati wa Kampeni zake mwaka 2012 
kwamba atafanya mabadiliko kwenye Katiba ili Rais akae madarakani kwa 
miaka mitano badala ya saba.
No comments:
Post a Comment