Wednesday, March 18, 2015

KUMBE KUNA MARAIS WANATAKA KUPUNGUZIWA MADARAKA? ISHU IKO HAPA

Kumbe kuna Marais wanaoomba kupunguziwa muda wa kukaa madarakani..!

RaisTuliona machafuko ya Burkina Faso ambayo yalitokana na ishu ya aliyekuwa Rais wa nchi hiyo, Blaise Compaoré kutaka kulishawishi Bunge ili limuongezee muda wa kukaa madarakani, iko ishu ya Congo DRC pia kwa sasa ambapo hali si shwari kutokana na machafuko ambayo yalianza baada ya Serikali ya nchi hiyo kutaka kufanya sensa ya watu na kusogeza mbele muda wa kufanya Uchaguzi Mkuu.
Stori za viongozi wa Afrika kujiongezea muda wa kukaa madarakani ni kawaida kusikika, lakini kusikia kwambe eti Rais wa nchi anaomba kupunguziwa muda wa kukaa madarakani hii imekaa tofauti mtu wangu!
Rais wa Senegal, Macky Sall amependekeza ipigwe kura ya maoni ambayo itafanya kuwe na mabadiliko ya Katiba ambayo yatafanya muda wake wa kukaa madarakani upungue kutoka miaka saba kwa muhula mmoja wa uongozi mpaka miaka mitano.
Rais huyo amesema alichaguliwa kwa miaka saba lakini mwakani mwezi Mei anapendekeza kufanyika kwa kura ya maamuzi ili kupunguza kwa muda wake na kupisha wengine waendelee na nafasi hiyo.
Kama hili likitimia Rais Sall atakuwa ametimiza moja ya ahadi aliyoahidi wakati wa Kampeni zake mwaka 2012 kwamba atafanya mabadiliko kwenye Katiba ili Rais akae madarakani kwa miaka mitano badala ya saba.

No comments:

Post a Comment